Wednesday, March 18, 2015

LUNGI ADAIWA KUTUPIWA JINI, APOOZA

NYOTA wa filamu za Kibongo Lungi Maulanga hivi karibuni anadaiwa kutupiwa jini na wabaya wake wakiwemo wanafamilia yake kitendo kilichosababisha apooze upande mmoja wa mwili wake.

Nyota wa filamu za Kibongo Lungi Maulanga.
Chanzo makini kinasema hofu yao kubwa ni kuwa kitendo hicho kilifanywa na baadhi ya ndugu zake kufuatia tofauti zao za kifamilia zilizosababisha kufikishana mahakamani.
“Katika shauri hilo mahakamani, yeye alishinda, sasa baada ya siku mbili akaanguka na kupoteza fahamu, alipozinduka akajikuta amepooza upande wa kulia, watu wanaunganisha tukio hilo na kesi ya mahakamani,” kilisema chanzo.
Gazeti hili lilimkuta Lungi akiwa amelala nyumbani kwake na alikiri kuanguka na kupooza na kwamba hawezi kutembea vizuri lakini anamtumaini Mungu kuwa hali yake itakaa vizuri kwani hana imani na mambo ya kishirikina.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...