BAADA ya tetesi kuzagaa kwamba Mtangazaji wa Clouds
TV, Benny Kinyaiya anafanya biashara haramu ya kuuza madawa ya kulevya
‘unga’ ambapo husafiri mara kwa mara kinyemela kwenda Ulaya, mwenyewe
amefungukia tuhuma hizo.
Akichati na gazeti hili juzi akiwa nchini Uingereza, Benny alisema
kuwa anashangazwa na madai hayo kwani hajawahi na wala hafikirii kufanya
biashara hiyo.
“Hizo taarifa ni za uongo kabisa, ni kweli nasafiri mara kwa mara na
hata sasa niko Ulaya kwa biashara zangu binafsi lakini hilo la unga siyo
kweli, ni uzushi tu. Kuna mambo yangu ya kibiashara nakuja kufanya
ambayo siwezi kuyaanika,” alisema Benny.
No comments:
Post a Comment