Tuesday, February 10, 2015

NGASSA ATANGAZA RASMI KUONDOKA YANGA



 
Ngassa katikati akiwa na Mkuu wa Idara ya Habari wa Yanga, Jerry Murro kushoto kwake.
Kiungo mshambuliaji wa Yanga, amekata mzizi wa fitina baada ya kusema kuwa hana matarajio ya kusaini mkataba mwingine katika klabu za Tanzania badala yake anataka kucheza soka la nje iwapo mkataba wake utakwisha mwishoni mwa msimu huu.
Ngassa mkataba wake umebakiza miezi mitano kumalizika, ambapo bado hajasaini na amesema kuwa ndoto zake ni kucheza kimataifa zaidi na kwamba katu hawezi kusaini katika klabu za hapa. Hata hivyo uongozi wa Yanga kupitia kwa Mkuu wa Idara ya Habari wa Yanga, Jerry Murro ulisema hawapo
tayari kumuachia kutokana na umuhimu wake klabuni hapo kwa sasa.
“Bado nina mkataba na Yanga na nitaendelea kuitumikia, lakini Inshallah sitasaini tena timu za hapa, nitaangalia mbele zaidi,” alisema Ngassa katika mkutano wa waandishi wa habari.
Kauli yake, inaaksi taarifa za kwamba nyota huyo alikuja kuaaga mashabiki wa Yanga baada ya  kuifungia timu yake mabao mawili ya ushindi kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar Jumapili na kuiwezesha timu hiyo kukaa kileleni kwa pointi 25, tatu zaidi ya Azam.
Ngassa mwenye jezi ya kijani, akidhibitiwa vilivyo na aliyekuwa beki wa Manchester United, Fabio Da Silva wakati akiwa na kikosi cha Seatle Sounders ya Marekani mwaka 2012.

Taarifa zaidi zinasema kuwa nyota huyo ana dili la kujiunga na klabu ya El Merreikh ya Sudan na ndiyo maana hataki kuingeza mkataba licha ya uongozi wa klabu hiyo kutangaza kutaka kuanza mchakato wa kumuongezea mwingine pamoja na wachezaji wengine wanaomaliza mikataba mwishoni mwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...