Friday, January 30, 2015

KEKI YA JOKATE, YAMZULIA JAMBO MILLARD AYO


Keki iliyoandaliwa na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kwa ajili ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ‘bethidei’ ya Millard Ayo ‘Mtu wa Nguvu’ imeibua mambo kwa mashabiki wao.
TUJIUNGE NA MILLARD
Ishu hiyo ilijiri Januari 26, mwaka huu ambapo Jokate alimpekea keki ofisini kwake Mikocheni jijini Dar, na kujumuika na jamaa zake kukata keki hiyo.
Kwenye pati hiyo, Millard ambaye ni mtangazaji mkali wa Vipindi vya Amplifaya na Top 20 vya Clouds FM, alidaiwa kumwalika Jokate ambaye mashabiki wao walimpa jina la Special Girl (msichana maalum).Pia katika pati hiyo, ‘ubuyu’ ulienea kwamba Jokate ndiye aliyekaangariza madikodiko na 
kupakua nyumbani kwa jamaa huyo kisha akamwandalia bonge la keki.
WALISHANA KEKI, JOKATE AONA AIBUHata hivyo, picha zao za kimahaba wakilishana keki hiyo zilizidi kuzua gumzo huku Jokate ambaye ni mwanamitindo na mwigizaji wa sinema za Kibongo akionekana mwenye aibu.

“Wamependeza sana wakati wakilishana keki, hongera zao,” ilisomeka sehemu ya maoni lukuki kwenye mitandao ya kijamii.
JOKATE ABANWA 
Ili kuondoa utata juu ya uhusiano wa Jokate na Millard, Ijumaa lilizungumza nao ambapo kila mmoja aliweka mambo hadharani.
 Ijumaa: Haloo Jokate…
Jokate: Haloo Hamida (mwandishi)...mambo vipi? Ijumaa: Poa. Kuna ishu naomba nikuulize inahusiana na uhusiano wako na Millard…

Jokate: Nini tena jamani?

Ijumaa: Kuna taarifa kwamba wewe ndiye uliyemwandalia Millard pati ya birthday na bonge la keki, je, ni kweli?

Jokate: Hamna. Millard is my friend tu…

Ijumaa: Inasemekana mbali na keki uliyompelekea pia ulimpikia. Je, hii imekaaje?

Jokate: Sikumpikia yeye.
Ijumaa: Sasa ulimpikia nani?

Jokate: Nilipika nyumbani tu, niliwapikia ndugu zangu.

Ijumaa: Vipi kuhusu keki ambayo ulimpelekea?

Jokate: Keki nilimpelekea zawadi cause anafanya vizuri.

Ijumaa: Mbona sisi tunafanya kazi nzuri na birthday zinapita hujawahi kutuletea?

Jokate: Niliamua tu.
Ijumaa: Wewe tunajua upo singo, je, yeye ana girl friend na unamjua?

Jokate: Hilo swali muulizeni yeye kwani ni kitu personal (binafsi).

Ijumaa: Hivi unajua wewe ni beautiful na yeye ni handsome?

Jokate: Kumbe mzuri eee…hahahahaa.

Ijumaa: Basi poa mtu wa nguvu.
Jokate: Poaaa…

BOFYA HAPA KUMSIKIA MILLARD


Baada ya kumsikia Jokate, Ijumaa lilimgeukia Millard ambapo mahojiano yalikuwa hivi;

Ijumaa: Mambo Millard.

Millard: Poa mambo vipi?
Ijumaa: Poa, kuna taarifa inasambaa kwa kasi kuwa wewe na Jokate mnatoka baada ya kukuletea bonge la keki siku ya bethidei yako. Unalizungumziaje?

Millard: Siyo kweli kama watu wanavyosema. Kama vipi wapotezee.

Ijumaa: Lakini mbona hata sisi tunasikia ni wapenzi?

Millard: Watu wanazusha tu lakini siyo hivyo.
Ijumaa: Lakini ni kweli amekufanyia pati ya bethidei na lile keki?
Millard: Kwanza haikuwa pati kihivyo. Ilikuwa ishu ndogo tu ya nyumbani. Jokate alihudhuria tu kama rafiki na siyo kama watu wanavyozusha.
Ijumaa: Mbona kuna picha za tukio zinakuonesha wewe na yeye? 
Millard: Ni picha tu ila hakuna chochote. 
NENO LA MHARIRI
Jokate na Millard vijana watafutaji ambapo Millard ni mtangazaji ‘jembe’ ambaye ni mfano wa kuigwa kwani amejijengea heshima kubwa ndani na nje ya Bongo hivyo kujikusanyia mashabiki wengi. Ijumaa linawapa hongera na kuwataka wazidi kupasua mawingu.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...