Friday, March 21, 2014

BATULI AJIWEKA KWA CHIEF KIUMBE



Staa wa filamu Yobunesh Yusuph ‘Batuli’ amedaiwa kujiweka kwa Pedeshee Chifu Kiumbe baada ya siku kadhaa zilizopita kumfuata na kumtaka amsaidie katika project ya filamu yake .
Staa wa filamu Yobunesh Yusuph ‘Batuli’.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, baada ya msanii huyo kupewa sapoti ikiwa ni pamoja na gari la kushutia, mdada huyo amekuwa akijionesha kuwa pedeshee huyo ni mtu wake.

“Alipopewa sapoti hiyo akaona ndiyo ajiweke kabisa bila kujua kuwa Chifu Kiumbe alikuwa akimsaidia tu na wala hakuwa na wazo la kumtaka,” alidai sosi huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.
 
Pedeshee Chifu Kiumbe.
Baada ya habari hizi kunaswa, mapaparazi wetu walimtafuta pedeshehe huyo ambaye alisema: “Hata mimi nashangaa kusikia watu wakisema natoka na yule dada, ukweli sijawahi kuwa mpenzi wake alikuja kuniomba msaada wa project yake nikamsaidia hata gari nilimpatia lakini nimesikia eti ananiita bebi kwenye mitandao ya kijamii, siyo kweli kabisa.”
Batuli.
Batuli naye anasemaje? Huyu hapa: “Mh! Watu wananisema mengi sana, waache waseme, mimi naongea na Chifu kawaida tu, hata jana nilimfuata anisaidie kama wasanii wengine.”

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...