Saturday, February 1, 2014

PENNY ZINGATIA PONGEZI HIZI NA ULIYOAMBIWA ILI UISHI KWA AMANI


Stori: Anko Nangale
LEO nabonga naye mwanadashosti anayeuza nyago kwenye kichupa cha DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Nianze kwa kukupa gwala kiroho safi. Juzikati umefunguka kuwa umepiga chini kiaina malovee na Diamond, mzuka mwingi. Umetisha sana.

Unajua laifu la malavidavi ndivyo lilivyo siku hizi. Mizinguo inakuwa mingi na wengi huwa wanatambua kuna taimu inafika unalazimika kupiga chini ili michongo mingine iendelee.

Nikiwa katika mingo zangu za kusaka chambi, nilipata bahati ya kuchonga na masela f’lani hivi ambao walikuwa wakizimikia penzi lenu, walipenda kuliona linakimbiza kitaa deile lakini wakasema umechagua bega sahihi, kubwaga manyanga kwa pisi.
“Ni uamuzi mzuri sababu mchizi akiwa hasomeki huna haja kufosi kingi wakati unaona hivihivi chombo kishaenda mrama, halafu mbona mtoto mwenyewe full mauzo, shepu anayo na ameumbika kinoma?” alifunguka mwana mmko.

Kwa wale ambao hatuko pamoko, msiogope. Ishu ilikuwa hivi, mapema wiki hii Penny alibonga na midia na akafunguka kuwa hamchukii ex wake huyo lakini wameamua kupeana spesi kiaina ili kila mmko wao aweze kufanya yake bila kupeana bugdha.

Penzi lao lilikuwa na tensheni ya kufa mtu, mingo zao za kimahaba zilikuwa zinasanuka kila kukicha. Baadhi ya wana walikuwa hawazimiki na skendo zako, ziliwaboa kinoma lakini hawakuwa na sehemu ya kufikisha meseji zao, waliamua kupiga kimya kimtindo.
Kwenye midia ulifunguka kuwa kama ikitokea umepata doni mpya, hutamaindi awe mtu maarufu, hicho ndicho wana wengi walichokitolea saluti. Wameona mafahari wawili hamuwezi kuishi kwenye zizi moko.
Kabla sijamaliza, nikupe salamu za watoto wa kishua kule kipande cha Oysterbay, Masaki na Mikocheni. Nao walizimika sana na yai lako, walipenda unavyodondosha ung’eng’e katika mahojiano yako ya mtandaoni.

Kimsingi ulienda nao sawa, walikuelewa kinoma. Ulipokuwa ukitema yai, wengi walikuwa wakiwatonya matha zao, si unajua zile za; “dadi, yu noo, shi izi andastendi…!” walifunguka kwa matha zao.
Walizimikia msimamo wako na kutamani wakupe tano hata la mbali.
Siyo kesi, chapa ilale umeshachagua bega. Spesi mmepeana, kamata kiburudisho kipya na muvi jipya liendelee.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...