Thursday, January 16, 2014

HATIMAYE LIYUMBA ASHINDA KESI YAKE YA KUKUTWA NA SIMU GEREZANI

Amatus Liyumba.

MKURUGENZI
wa zamani wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ameshinda kesi ya kukutwa na simu gerezani iliyokuwa inamkabili hivi punde katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Liyumba ameshinda kesi hiyo baada ya upande wa Jamhuri na mchunguzi wa kesi hiyo kushindwa kuithibitishia mahakama kuhusu tuhuma hiyo. Hukumu hiyo imesomwa na Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando kuanzia saa 3:30 mpaka 4:20 asubuhi.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...