Mkurugenzi wa
Vipindi na Maendeleo wa Clouds Group Ruge Mtahaba, akijaribu naye kutumia
uzowefu wake kwa kuwaonyesha wakazi wa Morogoro namna ya kutumia Fursa zilizopo
mkoani hapo.
SEMINA ya Kamata
Fursa Twenzetu inayotolewa na timu ya Serengeti Fiesta 2013, kila mkoa inapotua
burudani hiyo, leo imeendelea tena kujenga na kupanua mawazo ya wakazi wa
Morogoro katika mpango wa kuwawezesha kujua namna ya kutumia fursa zilizopo
mkoani hapo katika kujikwamua kwenye maisha yao.
Semina hiyo ilifanyika
mapema leo katika Ukumbi uliopo katika Hoteli ya Midland mjini Morogoro, ambapo
baadhi ya wataalam kutoka sehemu mbalimbali walipata muda wa kuzungumza na
wakazi hao na kuwajenga kwa kuwaonyesha njia mbalimbali za kujikwamua kimaisha.
Baadhi ya wakazi wa Morogoro waliokuwa
wamehudhuria ukumbini hapo wakifuatilia kwa makini semina hiyo.
Meneja wa
ujasiliamali wa Zantel Haidar Chamshama,akiwaonyesha wakazi wa Morogoro namna
ya kutumia fursa ya kubana matumizi kwa upande wa utumiaji wa simu za mkononi
na kujua faida za simu zaidi katika kujikwamua kimaisha.
Mkuu wa maswala ya
utafiti wa Maxcom Africa Ahmed S Lussasi, akiwafafnulia wakazi wa Morogoro
namna wanavyoweza kufaidika na bidhaa za Maxcom katika kujikwamua kimaisha.
Mtangazaji wa
Kipindi cha Sport Extra cha Clouds FM,Shaffi Dauda akionyesha namna ya kutumia fursa kwa upande wa michezo.
Mbunifu wa Mavazi
wa Morogoro,Diana Magesa (kushoto),akizungumzia fursa ya mambo ya ubunifu,huku
akionyesha na mavazi yake kwa kumvisha Mtangazaji wa kipindi cha Power
Breakfast cha Clouds FM, Jerald Hando, ambaye alikuwa mshereheshaji wa semina
hiyo.
Mwakilishi wa NSSF
kutoka Makao Makuu, Salim Khalifani akizungumzia namna ya kutumia fursa
zinazotokana na mafao ya NSSF kwa wakazi wa Morogoro leo ndani ya Ukumbi wa
Midland Hoteli mjini Morogoro.
Ruge akihitimisha
Semina hiyo kwa kukaribisha maswali kutokana na mafunzo waliyoyapata wakazi wa
Morogoro walihudhuria kwenye semina ya Kamata Fursa Twenzetu mapema leo.
Baadhi ya wakazi
waliokuwa ndani ya ukumbi huo wakiwa wamesimama baada ya kuombwa kuimba wimbo
wa Tanzania na Mrisho Mpoto kabla ya kuanza kuonyesha fursa kupitia sanaa yake
ya Muziki wa Kughani Mashairi.
Msanii wa Kughani Mashairi Mrisho Mpoto
akiwaimbisha wimbo wa Tanzania wakazi wa Morogoro muda mfupi kabla ya kuanza
kutoa njia za kutumia fursa kupitia sanaa ya muziki.
No comments:
Post a Comment