Monday, July 22, 2013


MSANII SHETTA AMALIZA BIFU NA BABA YAKE BAADA YA KUZINGUANA TANGU AKIWA NA MIAKA 7

 
Baraka za mwezi Mtukufu wa Ramadhan zimeitembelea familia ya Baba Qayllah, Shetta Bilal. Baada ya miaka mingi ya maelewano hafifu na baba yake mzazi, jana baba na mwanae wameamua kusameheana

Kupitia Instagram, Shetta amepost picha (hiyo juu) akiwa na baba yake mzazi Mzee Bilal ambaye ni Sheikh, pamoja na mdogo wake Awab na kuandika: Wit my daddy n my young broda Awab….. #happyday baada ya miaka mingi kuwa na tofauti na mzee tangu nina miaka 7 ljana yameisha #bassawa #Ramadankareem.”

Mwandishi wetu amezungumza kwa simu na Shetta kutaka kupata maelezo zaidi ya kwanini alikuwa haelewani na baba yake.
“Basi tu tulikuwa tunakosana, nahisi situations zangu na maisha yangu vilikuwa haviko sawa. Kazi yangu ninayofanya na nini kwasababu yeye ni mtu wa dini sana, baba yangu ni Al Haj, Sheikh. Kwahiyo nahisi hilo lilikuwa tatizo kwa upande wake..”


Shetta amesema kwa muda wote huo baba yake alikuwa hamfahamu mke wake pamoja mwanae, Qayllah lakini sasa anafuraha kwakuwa wameyamaliza baba yake amemuelewa.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...