Monday, July 22, 2013

KUNDI LA SCOPION GIRLZ KWISHA HABARI YAKE,SASA VIPANDE VIPANDE..WATUPIANA NGUO NJE

MEMBA wa Kundi la Scorpion Girls, Isabela Mpanda ‘Bela’ na Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ wametofautiana hadi kufikia hatua ya kutukanana na kutupiana nguo nje.
Mpango mzima ulitokea hivi karibuni Kijitonyama jijini Dar, nyumbani kwa Isabela ambapo chanzo cha ugomvi huo ni baada ya Isabela kumsifia mtandaoni X-memba wa kundi lao, Jacqueline Pentezel ‘Jack wa Chuz’ kwa kununua gari, ndipo Kabula alipokasirika na kuanza kumtukana Bela na mama yake matusi ya nguoni.
“Sikumuelewa kabisa Jini, kumsifia Jack kuhusu kumiliki gari ndiyo kumemfanya anitukane? Iliniuma sana na sitamsamehe, bora kila mtu achukue hamsini zake, nguo zake nilimtupia nje,” alisema Bela na kusisitiza kufanya muziki peke yake kwa sasa

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...