Monday, June 24, 2013

MAAJABU: MTOTO AZALIWA NA MAKALIO MATATU, MAMA YAKE ALIA AKIOMBA MSAADA



Maajabu ya uumbaji yamemfanya mama mzazi wa Xiao Wei ambaye ni mchina amwage machozi akiomba msaada wa kunusuru maisha ya mwanae mwenye umri wa miezi 7 aliyezaliwa na makalio matatu...
Kalio la tatu lipo kama mkia mfupi, wenye urefu wa sentimita 8 ( 8 cm ), katikati ya makalio mengine mawili.

Akiongea kwa uchungu, mama mzazi wa mtoto huyo amedai kuwa kwa muda mrefu amekuwa akiwaomba madaktari wafanye upasuaji wa tako hilo lakini wao wamekuwa wakimjibu kuwa hiyo si kazi nyepesi kama anavyodhani....

"Tukilikata litaota tena, hivyo hatutakiwi kukurupuka na badala yake tutakiwa kupata muda wa kupitia vitu vingi ukiwemo mrija wa uti wa mgongo ambapo kalio hilo limejiegesha"...Alisema daktari mmoja akimjibu mama huyo

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...