Tuesday, April 16, 2013

"MBUNGE ATAKAYETUKANA MATUSI YA NGUONI NITAMPELEKA POLISI".....SPIKA WA BUNGE



Akiongea kwa uchungu , Spika wa Bunge bi Anne Makinda amewashambulia wabunge leo asubuhi na kuwaambia suti zao walizovaa haziendani na matusi yanatoka katika vinywa vyao ambayo yeye ameshindwa kuyataja kutokana kwa madai kuwa mdomo wake hauwezi kutamka matusi hayo.....


Makinda amesema matusi ndiyo yamekuwa yakitawala katika midomo ya wawakilishi hao na kuacha hoja inayojadiliwa hewani....

Spika wa bunge amekwenda mbali zaidi na kuwaambia wabunge hao kwamba hataangalia chama endapo mbunge atavunja kanuni za bunge kwa kuwa kanuni za bunge zinampa nafasi ya kuita polisi na kuja kumchukua mbunge huyo kwa hatua za kisheria.

Makinda amesema ametumiwa sms ambayo mtumaji amedai hatokaa tena na familia yake kuangalia bunge labda ajifungie chumbani.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...