Tuesday, March 5, 2013

MTOTO ALIYEZALIWA NA VIRUSI VYA UKIMWI APONA...



Wanasayansi wametangaza kuwa mtoto aliyekuwa amezaliwa na virusi vinavyosababisha Ukimwi amepona na hana tena virusi hivyo.

Mtoto huyo wa huko Mississippi nchini Marekani amekuwa akitumia dawa kwa mwaka sasa na haoneshi kuwa na maambukizi hayo tena.

Hata hivyo hakuna uhakika asilimia 100 kuwa mtoto huyo amepona kabisa lakini vipimo vya hali ya juu vimetoka kumpima na haoneshi kuwa na virusi tena.

Habari hii inaweza kuwa mwanzo wa kupatikana tiba ya ugonjwa huo unaosababisha vifo vya watu wengi hususan barani Afrika.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...