Thursday, January 24, 2013

Tanzania ya pongezwa kwa kutatua migogoro Afrika


Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda akiwasili leo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kupokelewa na Kaimu Balozi wa Tanzania nchini humo Bwana Hemed Mgaza (katikati) Kushoto ni Mwenyekiti wa Bunge na Makanu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Musa Azzan Zungu (Mb). Kulia ni Mhe. Sadifa Juma Khamis, (Mb).Mhe. Spika ameongoza ujumbe wa Wabunge watano kuhudhuria Mkutano wa tatu wa Kimataifa wa Jukwaa la Kibunge la nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.


Spika Makinda na Spika wa Kenya Mhe. Kenneth Marende (kulia) wakiingia kwanye mkutano huo.

Ufunguzi wa mkutano wa Tatu wa PF –ICGLR (Forum of Parliaments of International Conference on Great Lakes Region – FP/ICGLR) mjini Kinshasa.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.

Picha ya pamoja ya maspika, Sekretarieti pamoja washirika wa maendeleo wa FP-ICGLR.
Jukwaa la Mabunge ya Jumuiya ya Kimataifa ya nchi za Ukanda wa Maziwa Mkuu (FP-ICGLR) limeitaja Tanzania kuwa mfano wa kuigwa kwa juhudi inazozifanya kuleta amani barani Afrika.

Pongezii hizo zimetolewa leo na jumla ya nchi wa kumi na mbili zinazounda Jukwaa hilo kwenye mkutano wa tatu unaoendelea kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zimewataja Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoa na watanzania kama wapenda amani barani Afrika

Hii ni kutokana na viongozi hao kujitolea kusuluhisha migogoro ya DRC/Rwanda na kundi la M23, migogoro ya Afrika ya Kati, mgogoro wa Sudani na Sudani Kusini, mgogoro wa Kenya baada ya uchaguzi mkuu na mingine mingi. Pamoja na Tanzania, Afrika Kusini nay imepongezwa

. Bunge la Tanzania limewakilishwa na Spika wa Bunge ambaye ameongoza ujumbe wa wabunge watano ambao ni Mhe. Mussa Azzan Zunge, Mhe. Pauline Gekul, na Mhe Sadifa Juma. Wengine ni Mhe. Mohamed Mbarouk na Mhe. Prudenciana Kikwembe.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...