Friday, January 4, 2013

SAFARI YA MWISHO YA MAREHEMU SAJUKI..








Waombolezaji wa Msiba wa Msanii wa Filamu hapa nchini,Marehemu Sadick Juma Kilowoko wakibeba jeneza lenye mwili wake tayari kwa taratibu za kwenda Mazikoni,wakitokea Nyumbani kwa Marehemu Tabata Bima.

Sasa hivi mwili wa Marehemu upo katika Msikiti wa Sheahk Adhir,Kariakoo kwa ibada ya Kusalia Mwili na baada ya Swala ya Ijumaa,Mwili utazikwa kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mwili ukipakiwa kwenye gari.

Dua ikisomwa kabla ya kuondoka na Mwili wa Marehemu kwenda mazikoni.

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania,Saimon Mwakifwamba akimpokea Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe alipokuwa akiwasili msibani hapo.



Waombolezaji wakiwa Msibani mapema asubuhi hii.




Pamoja na kwamba kulikuwa na Mvua kubwa lakini hakuna alitaka kuondoka msibani hapo mpaka pale mwili ulipoondoka kuelekea Msikitini kwa Kusalia na baadae kwenye Mazishi.

Mwili ukiondoka nyumbani.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...