Friday, December 28, 2012

WASANII DAYNA NA RICH MAVOKO WAWASHUKURU WATANZANIA



Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Mwanaisha Nyange a.k.a Dyana akiongea na waandishi wa habari (hawapo) pichani Dec, 28,2012 jijini Dar es Salaam, ametoa shukrani zake kwa Aljazerra Entertaiment kwa kumsaidia kumtoa msanii huyo kimuziki, bila ya kuwasahau, wadau mbalimbali wote wa muziki nchini ambao amesema ndio waliomsaidia kumfikisha hapo alipo sasa katika sanaa hii ya muziki huu wa kizazi kipya, kwani bila ya kupata ushirikiano wao asingeweza kufikia hapa alipo. (kushoto) ni Msemaji wa Aljazerra Entertaiment Simon John.

Msanii Richard Lusinga (a.k.a – Richie Mavoko) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani Dec,28,2012 jijini Dar es Salaam, wakati akitoa shukrani kwa niaba ya Kampuni yake ya Aljazerra Entertaiment, katika shukurani zake amesema,” kama msanii wa kizazi kipya amewaomba radhi kwa wote aliowakosea na yeye pia amewasemehe” Pamoja na Kushukuru kampuni ya Aljazerra Entertaiment, waandishi wa habari na wadau wote wa muziki nchini, kwani ndio waliomfikisha hapo alipofikia na kuahihidi atazidi kuboresha na kuwaletea nyimbo kali zaidi washabiki wake katika mwaka wa 2013. Richie Mavoko anatamba na nyimbo zake kama Mbona silai, Folo folo me, one time na Merry me . (kushoto ) Ni Msanii Mwanaisha Nyange (a.k.a DYANA).

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...