Monday, August 27, 2012

SIMBA SC WATEMBELEA KIWANDA CHA TBL ARUSHA


Mratibu wa Usalama na Afya wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kassena Heavy, akiwaeleza jambo wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba waliotembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu. 
 
TIMU ya Simba Sports Club ambayo imeweka kambi mkoani Arusha imefanya ziara ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza bia cha TBL kilichopo jijini hapa.
Akiongea katika ziara hiyo mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa timu hiyo, Ibrahimu Masoud Maestro, alisema kuwa wao kama timu ya Simba wameamua kufanya ziara yao katika kiwanda hicho ili kuweza kujionea mambo mbalimbali ambayo yanafanywa na kampuni hiyo inayozalisha bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio wadhamini wakuu wa timu yao.
Alisema kuwa Kilimanjaro Premium Lager imekuwa ikiwapa ushirikiano mkubwa katika mambo mbalimbali ya kimichezo ikiwa ni pamoja na kuwapatia magari ya usafiri jezi pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo hivyo wamefurahishwa sana na jinsi walivyopokelewa vizuri kiwandani hapo na aliwaomba waendelee na moyo huo huo wa kuthamini timu yao.
Akiongea kwa niaba ya kampuni hiyo Meneja wa bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema kuwa wamefurahishwa sana na kitendo hiki cha timu hii ya Simba kuamua kuacha shughuli zao na kutembelea kiwanda chao na kuona kazi ambazo zinafanywa na kampuni hii.
Alisema kuwa TBL inathamini mchango wa timu za Simba na Yanga kwa soka la Tanzania na ndio maana imekuwa ikizidhamini timu hizi kwa muda mrefu huku akibainisha kuwa wataendelea kudhamini timu hizi hadi mwisho.
Alibainisha kuwa timu hizi mbili zimekuwa zikifanya mambo makubwa kwani zimekuwa zikiwapatia vijana mbalimbali ajira kwa kupitia timu zao.
Aliwasihi wananchi kwa ujumla kuendelea kuisapoti timu hizi kwani ndio timu mbazo zina wachezaji wengi zaidi wanaochezea timu ya taifa.
Kavishe alisema kuwa kupitia kudhamini timu hizi pia wamekuwa wakijitangaza sehemu mbalimbali kwani iwapo timu ikienda kucheza nje ya nchi wanaenda kukitangaza kinywaji chake cha Kilimanjaro Premium Lager hivyo wanafanya kampuni hii pamoja na bia ya Kilimanjaro kuwa juu zaidi. 

 
 Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akiongea na wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba waliotembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
Meneja wa Mauzo wa Kanda ya Kaskazini wa kampuni ya bia Tanzania (TBL), Kasiro Msangi akiongea na wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba waliotembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
Wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba wakitembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
Kocha Mkuu wa Simba, Profesa Milovan Cirkovic akiongea na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe kwenye hafla iliyofanyika baada ya wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba kutembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
Wachezaji wa klabu ya Simba wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu.
Kocha Mkuu wa Simba, Profesa Milovan Cirkovic akitoa neon la shukrani baada ya wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba kutembelea kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu. Kulia kwake ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe na Meneja wa Vifaa wa Klabu ya Simba, Kessy Hassan (kushoto)

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...