Monday, August 6, 2012

MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA ILALA JERRY SILAA ARUDISHA FOMU ZA UVCCM - NEC


Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilala Jerry Silaa akirejesha fomu za kugombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC kwa katibu wa UVCCM mkoani Mwanza. Bw. Elias Mpanda, katika ofisi za CCM mkoani- Jijini Mwanza. Mstahiki meya Manispaa ya Ilala Bw. Jerry Silaa anagombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC ngazi ya taifa.

Mstahiki meya aliweka wazi nia yake ya kutaka kuwawakilisha vema vijana wa Kitanzania kwenye UVCCM-NEC na aliwaasa vijana wengine kushiriki kwenye mchakato huo na huku akisisitza kwamba yuko tayari kufanya kazi kokote nchini kwa maslahi ya wananchi, vilevile meya aliwaasa viongozi wote kuwajibika na kutimiza ahadi zao walizozitoa kwa wananchi na kwa kuweka mbele maslahi ya taifa na sio yao.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...