Tuesday, August 14, 2012

‘MERCEDES CUP 2012′ YASISIMUA FUKWE DAR



Baadhi ya picha za boti zinazotumika kwenye mashindano hayo ndani ya fukwe za Yatch Club jijini Dar es Salaam.

Washiriki wakichuana.

Boti iliyombeba Refarii wa mashindano hayo pamoja na wasimamizi wengine.

Tuzo za washindi zikiwa mezani.

Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed(katikati) akijadili jambo na Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh (kushoto) pamoja Catamaran Representative wa Dar es Salaam Yatch Club Andrew Boyd.

Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh (katikati) akizungumza machache baada ya kumalizika kwa mashindano hayo ambapo amewataka watu kujitokeza kwa wingi kila mwaka na kutoa shukrani zake kwa wote walioshiriki kufanikisha mashindano hayo. Kushoto ni Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed na kulia ni Andrew Boyg wa Dar es Salaam Yatch Club.

Washiriki na familia zao wakisubiri kuanza kwa zoezi la kutoa zawadi.

Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh akimkabidhi zawadi Refarii wa mashindano hayo.

Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh akikabidhi zawadi kwa moja ya timu iliyoshiriki mashindano hayo na kushika nafasi ya nne.

Washindi wa tatu David na Sarah Scott wakipokea zawadi na tuzo.

Pichani Juu na Chini Washindi wa pili Paul na Kim Troll wakipokea zawadi kutoka CFAO Motors.


Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed akikabidhi Kombe kwa timu ya washindi wa kwanza wa mashindano ya Boti zinazokwenda kwa kutumia upepo (Sailing Boat) ya Mercedes Cup 2012 Al Bush na Jeppe yaliyofanyika katika fukwe za Yatch Club Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh. Mashindano hayo yanayofanyika kila mwaka yamedhaminiwa na Kampuni ya CFAO Motors.

Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed akigawa Champagne kwa washindi.

Mshindi wa kwaza akifungua Champagne.

Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed (Kulia) na Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh (kushoto) katika picha ya pamoja ya washindi wa kwanza hadi wa tatu walioshiriki mashindano ya Boti zinazokwenda kwa upepo (Sailing Boat) ya Mercedes Cup 2012 baada ya kukabidhiwa vikombe na zawadi zao yaliyofanyika katika fukwe za Yatch Club jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Mashindano hayo yanayofanyika kila mwaka yamedhaminiwa na Kampuni ya CFAO Motors.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...