Monday, July 2, 2012

Mratibu na jaji wa shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012,Reuben Ndege a.k.a Ncha Kali kutoka Clouds FM,akimpa maelekezo mafupi Pacha Great mara baada ya kuibuka kinara wa shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa,kwa kuwashinda mahasimu wenzake wapatao 32 waliofika kushirika mchakato wa shindano hilo.shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa limeandaliwa na Prime Time Promotions/Clouds FM kwa udhamini mkubwa wa kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake murua kabisa cha Serengeti Premium Lager.




Majaji wa shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa wakijadiliana jambo,kutoka kulia ni JCB,Reuben Ndege a.k.a Ncha Kali kutoka Clouds FM pamoja na Mdau wa muziki wa hip hop,Mo-Plus.



Mashabiki wakishangilia jambo ukumbini humo.

 




Mratibu wa shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa,Adam Mchiomvu akitajana majina yaliyoingia fainali kwenye shindano hilo,ambalo limekuwa na msisimko mkubwa kwa vijana wengi wa jiji la Arusha,katika mchakato mzima wa shindano hilo walijitokeza vijana 32,wakachunjwa na kupatikana wengine 12,na hatimaye kuwapata sita ambao walishindana vikali,aidha katika sita hao aliihitajika kinara mmoja tu wa kughani kwa miondoko huru.




Mwanadada machachari kabisa aitwaye Tiger Eyes akionesha umahiri wake wa kughani mbele mashabiki waliofika kwenye shindano la kumsaka mkali wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...