Thursday, July 26, 2012

BAADA YA MV SKAGIT, HII NDIO TAARIFA RASMI YA AJALI NYINGINE YA JANA.




kama unakumbuka wakati MV SPICE ISLANDERS inazama muda mfupi baadae kuna jahazi la mizigo lilizama likitokea Tanga, sasa stori ya leo ni kwamba baada ya MV SKAGIT kuzama wiki iliyopita Jeshi la Polisi Zanzibar limethibitisha kuzama kwa Jahazi jumatano ya July 25 2012 siku saba baada ya ajali ya MV SKAGIT.

Msemaji wa Polisi Mohamed Mpinga amesema kwamba Jahazi lilikua linatokea Kusini Pemba kwenda Nungwi kaskazini Unguja ambapo mtoto wa miaka mitano Isaka Hamis alipoteza maisha.

Polisi mkoa wa Kusini Pemba wamesema chanzo cha ajali ni ujazaji wa mizigo uliopitiliza kwani Jahazi hilo lilibeba magunia kumi ya Muhogo, mikungu 10 ya ndizi pamoja na mizigo mingine ya kuni. Watu sita walinusurika kifo akiwemo mama mwenye mtoto wa miaka miwili, vyombo hivi vya uvuvi vimekua vikitumika kusafirisha abiria na mizigo kimakosa wakati pia havitakiwi kusafiri umbali mrefu.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...