Thursday, March 1, 2012

  DKT BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA MACHINJIO-IRINGA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka jiwe la msingi katika Jengo jipya la Machinjio lililojengwa katika Kijiji cha Ngelewala mkoani Iringa wakati akimalizia ziara yake katika mkoa huo jana Februari 29, 2012. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, C. Ishengoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Asha Bilal, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Kilimo na Mifugo wa Manispaa ya Mafinga, Augustino Nyenza, wakati akitoa maelezo kuhusu jengo jipya la Machinjio lililojengwa katika Kijiji cha Ngelewela mkoani Iringa, jana Februari 29, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya wachungaji wa mkoani Iringa, baada ya kumaliza majumuisho ya ziara yake katika mkoa huo jana Februari 29, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mbunge wa Jimbo la Iringa mjini, kupitia tiketi ya CHADEMA, Mchungaji Peter Msigwa, wakati akiwa Uwanja wa Ndege wa mkoani Iringa jana akirejea jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara yake ya mkoani humo.
 

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...