Friday, March 11, 2016

NAIBU WAZIRI WA KAZI, AJIRA NA VIJANA ATHONY MAVUNDE AZINDUA TAMTHILIA YA 'KELELE'

Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (wa saba kutoka kushoto), akiwa kwenye pozi la pamoja na baadhi ya washiriki wa tamthilia hiyo.

NAIBU Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, usiku wa kuamkia leo amefanikisha uzinduzi wa tamthilia mpya ya Kelele, iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuendeleza na Kukuza Vipaji (Tanzania House of Talent – THT).

Uzinduzi huo ulifanyika   ndani ya Ukumbi wa Paparazi uliopo katika Hoteli ya Slipway Masaki jijini Dar es Salaam.  Akizungumza muda mfupi kabla ya kuzindua tamthilia hiyo. Mavunde alisema kwamba, anawapongeza  THT kwa kuendelea kuisaidia serikali kwenye suala la kuwatafutia vijana ajira.

“Tunaishukuru sana THT kwa kuendelea kuiunga mkono serikali kwenye suala la kutatua na kuendelea kuongeza ajira kwa vijana wetu, tunatambua wazi kabisa kuwa serikali pekee haiwezi kumaliza tatizo hili pasipo watu binafsi kuongeza ajira kwa namna hii,” alisema Mavunde.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, alimpongeza Mavunde  kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa filamu hiyo.
Mavunde akiongea jambo wakati wa uzinduzi huo ukumbi wa Paparazi Masaki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, akielezea namna walivyoiandaa tamthilia hiyo.
Baadhi ya wanamitindo wakitoa burudani kwenye uzinduzi huo.
Msanii wa Hip Hop, Farid Kubanda ‘Fid-Q’ (katikati), akibadilishana mawazo na Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na Mtangazaji wa East Africa Radio, Ana Peter.
Baadi ya waimbaji wa THT Band wakitumbuiza kwenye uzinduzi huo.

Wasanii wanaounda kundi la Navy Kenzo, Nahreel na Aika wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Wanamitindo wakiwa katika pozi la pamoja baada ya kumaliza kutoa burudani.
Warembo wakiwa mbele ya kamera.
Mwana mitindo maarufu Bongo, Ally Rehmtulah, akiwa  na mrembo.
Mtangazaji wa Clouds TV, Shadee akiwa kwenye pozi kwenye Red Carpet.
Mtangazaji wa Clouds FM na TV, Hamisi Dakota.
Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na rafikiye.
Vijana wanauonda kundi la Makomando wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Baadhi ya wadau waliohudhuria uzinduzi huo wakibadilishana mawazo.


No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...