Tuesday, February 23, 2016

MZIMU WA OSTAZ JUMA NAMUSOMA WAZIDI KUWATESA WASANII HAWA!!

Miongoni mwa mameneja Tanzania waliosaidia kuusimamisha muziki wa Bongo Fleva na Dansi, Ostaz Juma Namusoma. 

UKIZUNGUMZIA miongoni mwa wadau wakubwa wa muziki waliosaidia kuusimamisha muziki wa Bongo Fleva na Dansi nchini ni wazi jina la Ostaz Juma Namusoma litakuwa miongoni mwa majina utakayoyataja.
Kabla ya kuwasimamia wanamuziki wa Bongo Fleva, Ostaz Juma Namusoma alikuwa akiwasaidia sana wanamuziki wa Dansi kama vile Ali Chocky, Super Nyamwela, Jose Mara, Kalala Junior, Nyoshi El-Saadat, Christian Bella, Mwinjuma Muumini na wengine wengi.
Ikumbukwe kuwa hata Wimbo wa Ubinadamu ulioimbwa na Christian Bella ulikuwa maalum kwa mdau huyo wa muziki. Ostaz Juma aliamua kuupa kisogo muziki wa Dansi na kujikita kwenye Bongo Fleva ambapo alianzisha Kampuni ya Watanashati iliyokuwa na vichwa kama vile, PNC, Marehemu Sharomilionea,Kitale, Suma Mnazareti pamoja na Dogo Janja.
Wasanii hao wote kwa sasa hawapo chini yake kutokana na kila mmoja kuondoka kwenye kampuni hiyo na huku nyuma yake akimwagia maneno mbofumbofu  na kejeli nyingi kwa mdau huyo na baada ya muda tangu watoke walijikuta wakishindwa kuendana na soko la muziki.
Katika makala haya yanawachambua wasanii hao ambao mzimu wa Ostaz Juma bado unazidi kuwatesa.
Msanii wa Bongo Fleva aliyewahi kuwa chini ya usimamizi wa Ostaz Juma Namusoma kupitia kampuni ya Mtanashati PNC  akiwa katika pozi.
PNC
Pancras Ndaki kama anavyojulikana kwenye cheti chake cha kuzaliwa, anaingia kwenye listi ya wasanii waliopitia kwenye mikono ya Ostaz Juma na kupata kusikika vilivyo.
PNC alikaa na Ostaz Juma kwa muda mrefu na kuamua kujitoa huku sababu akiitaja ni mambo kumwendea mrama kwa kuwa alikuwa akijaribu kutoa nyimbo za kila aina kulishawishi soko gumu la muziki wa Bongo Fleva lakini mambo hayakuwa sawa.
Aliamua achukue uamuzi mgumu wa kujiondoa na kuanzisha kundi la Top Fleva huku akidai alikuwa hapati msaada wowote kwa bosi wao (Ostaz Juma) na kwamba anawasema vibaya kwenye media. Baada ya kusema hayo tu miezi michache, PNC alirudi na kumpigia magoti Ostaz Juma kumuomba msamaha na kwamba amrudishe kundini.

Msanii aliyekuwa chini ya usimamaizi wa Ostaz Juma Namusoma kupitia kampuni ya Mtanashati Suma Mnazareti katika pozi.
Suma Mnazareti
Suma Mnazareti naye ni miongoni mwa wasanii wanaoendelea kuandamwa na mzimu wa Ostaz Juma baada ya kujitoa.
Kwa mujibu wa Suma, aliamua kujitoa kwa sababu alikuwa akikosa kile alichokuwa akitarajia na pia aliona kama Ostaz anawajali sana wasanii wa muziki wa Dansi japokuwa alikuwa amejikita kwenye Bongo Fleva.
Baada ya kujitoa kwake alifanikiwa kutoa wimbo na Ommy Dimpoz uitwao Chukua Time ukafanya poa sana kisha Tuko Wangapi akiwa na Tunda Man nao ukafanya poa huku akitoa vijembe kwa Ostaz Juma.
Baada ya hapo, mzimu wa Ostaz Juma ukaanza kumtesa na kujikuta akishindwa kurejea kwenye soko la muziki na kila kazi aliyokuwa akiitoa ilikuwa ikibuma hadi sasa.
Dogo Janja.
Dogo Janja
Abdulaziz Abubakari  ama Dogo Janja kwa jina la kisanii, alichukuliwa na Ostaz Juma baada ya kuachana na kundi la Tip Top ambapo alijiunga na wenzake ambao ni PNC pamoja na Suma Mnazareti na kufanikiwa kutoka na wimbo wa pamoja ulioitwa Watanashati.
Baada ya kukaa kwa kipindi kirefu, Dogo Janja alitimuliwa na Ostaz Juma kwa sababu iliyoelezwa ni kukosa heshima na pia kukimbiwa japokuwa alimtafutia shule ambayo alishindwa kusoma.
Dogo Janja aliamua kurudi Tip Top chini ya Madee lakini napo mzimu wa Ostaz Juma uliendelea kumtesa ambapo inaelezwa kuwa hadi sasa ameingia katika mtafaruko mkubwa baada ya kudai kuwa ana kazi zaidi ya 10 ambazo anabaniwa kuzitoa huku akirandaranda mitaani pasipo ishu yoyote.

Ostaz Juma Namusoma katika pozi.
Msikie Ostaz Juma
Over The Weekend ilifanikiwa kuzungumza na Ostaz Juma juu ya wasanii hao ambapo alifunguka;
“Ujue sisi wadau wa muziki huwa tunaandamwa sana na maneno hasa pale unapoachana na msanii uliyekuwa ukimsaidia. Nimewahi kuwasaidia wasanii wengi kwa mfano ukiangalia mimi na Fella (Said Fella) tunawasimamia wasanii kwa pesa zetu za mfukoni tofauti na mameneja  wengine ambao wamekuwa wanasimamia wasanii  kwa manufaa yao kama hawapati basi wanaachana na wewe.
“Wasanii hao (Suma, PNC na Dogo Janja) nawatambua kama wasanii waliopitia kwenye mikono yangu, japokuwa kila mmoja aliamua kuondoka lakini naendelea kuwasaida pale wanapokwama hadi leo.
Kweli juzikati nilibahatika kuwa miongoni mwa watanzania wengi niliyesikiliza sauti ya Dogo Janja akiongea na msaichana mmoja huku akitoa lawama kubwa kwa wasimamizi wake wa sasa ambao wamekuwa naye kwa muda mrefu sasa tangu atoke kwangu.

Record hiyo kweli imenisikitisha sana baada ya kumuona kijana wangu akilalama kiasi hicho lakini kikubwa nilichokigundua hapo ni kwamba, mameneja wengi wa wasanii wetu ni tatizo maana wamekuwa wakiwachukua wasanii ili wao wanufaike badala ya kuwasaidia kama nilivyokuwa nikifanya mimi na Said fella.

Kusema kweli kwa haya maneno ya Dogo Janja naanza kuona wazi kabisa kuwa Babu Tale na Madee hawana uwezo wa kummeneji msanii hasa asiyekuwa na fedha maana wao wanataka pesa kutoka kwake huku msanii mwenyewe amekuwa akihitaji msaada wa kikazi na fedha.
Boss wa Mtanashati Ostaz Juma Namusoma katika pozi.
Mimi suala la mzimu wangu kuwasumbua kweli nimekuwa nikiambiwa na wengi hata baadhi ya wasanii hawa kama PNC juzi kati aliwajhi kuniambia kitu kama hicho, tena akisema kweli mkono wangu si wakuacha vibaya kwani karibia wote niliowahi kuwasimamia wameshindwa kuendelea nje ya Mtanashati na zaidi wanmebaki wakitabika kama unavyomuona Dogo Janja leo hii.


PNC alikuwa akiniambia kuwa kwenye maisha jhakuna mtu asiyekuwa na mapungufu ila mimi kwake nitabaki kuwa kama lulu ya mafanikio kwani pamoja na yeye kutoka kwangu kwa mwembwe nyingi bado amekuwa akinihitaji kwa asilimia kubwa sambamba na wengine wote akiwemo Dogo Janja ambaye ninamsaidia anapokwama,” alisema Ostaz Juma.
Ostaz Juma Namusoma.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...