Thursday, July 16, 2015

MKUBWA FELA KUWANIA UDIWANI MBAGALA KWA TIKETI YA CCM

Fela (kulia) akikabidhiwa fomu za kugombea udiwani 
MKURUGENZI wa kundi la Yamoto Band, Said Fela leo amechukua fomu za kuwania udiwani katika Kata ya Kilungule, Mbagala, Temeke, Dar es Salaam.
Fela ambaye pia ni mwasisi wa kundi la TMK Wanaume Family na Mkurugenzi wa kituo cha Mkubwa na Wanawe kinachosimamia bendi ya vijana machachari wa Yamoto, ameamua kuchukua fomu hiyo na kugombea nafasi hiyo ili aweze kutatua kero za wakazi wa kata ya Kilungule na kuleta maendeleo katika Kata hiyo.
"Nimeamua kuchukua nafasi hii ili kutatua kero za kata yangu, hapa kuna shida ya maji na barara naamini nikiwa Diwana nitaweza kuonana na wakubwa wa nchi uso kwa uso,"amesema.
Mkubwa Fela akijaza fomu za kuwania Udiwani

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...