Saturday, June 6, 2015

WASTARA: ‘ALIYENIONJA’ AJITOKEZE

VUNJA ukimya! Baada ya kuhusishwa kwa muda mrefu na fununu za kutembea na wanaume kadhaa tangu kufariki kwa aliyekuwa mumewe, Juma Kilowoko ‘Sajuki’, msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma hatimaye amefunguka na kujiapiza kwa kulamba kidole, kuchovya mchanga na kukipitisha shingoni akidai tangu kuondoka kwa Sajuki hajawahi ‘kuchangia shuka’ na mwanaume yeyote na kama yupo, ajitokeze hadharani!
Msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma.
‘Akibadilishana sentensi’ na ‘kiruka’ njia wetu kwa njia ya simu hivi karibuni, Wastara ambaye bado anafanya vyema kwenye sanaa, alishutumu na kuonekana kuchukizwa vikali na tetesi juu yake akihusishwa na wanaume kadhaa akiwemo msanii mwenzake, Bond Bin  Suleiman.
“Nashangazwa sana na wanaoeneza uvumi wa mimi kutembea na wanaume wengi baada ya kifo cha mume wangu, kwani mimi sina haki kama mwanamke jamani? Kama kuna mwanaume mwenye uthibitisho wa kutembea na mimi si ajitokeze!” alisema Wastara huku akiashiria jazba.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...