VUNJA ukimya! Baada ya kuhusishwa kwa muda mrefu na
fununu za kutembea na wanaume kadhaa tangu kufariki kwa aliyekuwa
mumewe, Juma Kilowoko ‘Sajuki’, msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma
hatimaye amefunguka na kujiapiza kwa kulamba kidole, kuchovya mchanga na
kukipitisha shingoni akidai tangu kuondoka kwa Sajuki hajawahi
‘kuchangia shuka’ na mwanaume yeyote na kama yupo, ajitokeze hadharani!
‘Akibadilishana sentensi’ na ‘kiruka’ njia wetu kwa njia ya simu hivi
karibuni, Wastara ambaye bado anafanya vyema kwenye sanaa, alishutumu
na kuonekana kuchukizwa vikali na tetesi juu yake akihusishwa na wanaume
kadhaa akiwemo msanii mwenzake, Bond Bin Suleiman.
“Nashangazwa sana na wanaoeneza uvumi wa mimi kutembea na wanaume
wengi baada ya kifo cha mume wangu, kwani mimi sina haki kama mwanamke
jamani? Kama kuna mwanaume mwenye uthibitisho wa kutembea na mimi si
ajitokeze!” alisema Wastara huku akiashiria jazba.
No comments:
Post a Comment