Thursday, June 18, 2015

DAYNA ANASWA KIMAHABA!

PICHA za staa wa muziki wa Bongo Fleva, Mwanaisha Said ‘Dayna Nyange’ akiwa katika pozi la kimahaba zimenaswa.
Picha hizo zinazomuonesha akiwa katika ‘mabusu ya kiutuzima’ na mwanaume mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Mwanaisha Said ‘Dayna Nyange’.
Baada ya kunaswa kwa picha hizo, Amani lilimvutia waya Dayna ambapo alijitetea kuwa hajui picha hizo zimesambaaje japokuwa ni kweli alipiga akiwa na mchumba wake ambaye kwa sasa hayupo naye.
“Kuna kipindi jamaa yangu aliniambia kuwa simu yake imeharibika na ipo kwa fundi, sasa huenda walimfanyia mchezo mbaya,” alijitetea Dayna.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...