Lucy Mgina,Dar es Salaam
UTANASHATI
ni jambo kubwa sana kwa wasanii na watu wa kawaida. Mara nyingi
utanashati humtambulisha muhusika namna anavyojiweka kuanzia nyumbani
hadi katika mwili wake.Hapa Tanzania kuna wasanii kibao ambao wamekuwa
wakijitahidi kujiweka fresh kwa uvaaji wao na hilo limewafanya
kujiongezea umaarufu zaidi na sifa kujaa kwao.
Mara nyingi imekuwa ikichukuliwa kuwa watu wenye mkwanja ndiyo
wanatakiwa kupendeza, lakini siyo hivyo! Unaweza kuwa na fedha nyingi na
ukanunua kila aina ya nguo unayotaka lakini kitu kidogo tu
kikakuangusha ambacho ni kushindwa kupangilia rangi ya nguo au kutojua
uvae nini kwa wakati gani.
Wasanii wengi wa Bongo Fleva ambao leo ndiyo nawazungumzia wamekuwa
wakijitahidi kujiweka sawa, na hii ni kutokana na kuwa na mizunguko
mingi ya ndani na nje ya nchi hasa katika shoo, hivyo hupata fursa zaidi
za kujifunza huko.
Sasa wafuatao ni baadhi ya mastaa wa Bongo Fleva
ambao wanajua kupangilia mavazi yao na kufanya waonekane ng’aring’ari
muda wote wanapokuwa mbele ya jamii.
Jux
Juma Mussa maarufu kama Jux, ndiye msanii
anayeongoza kwenye utupiaji wa nguo zenye brand kali za aina mbalimbali
na huwa zinampendeza. Wapo wengi ambao wanavaa vizuri lakini Jux amekuwa
akiwavutia wengi kila anapoonekana kutokana na kutupia vyema mavazi
yake.
Anafanya muziki wa R&B na amekuwa akifananishwa zaidi na msanii
wa Marekani, Trey Songz katika uimbaji. Licha ya kuwa hajaoa (anatajwa
kutoka na msanii Vanessa Mdee) lakini linapokuja suala la mavazi jamaa
ni msafi na anajua kupangilia hiyo yote inasababishwa na yeye mwenyewe.
Kamikaze ‘Cyril’
Anafahamika zaidi kwa jina la
Cyril ambapo alilazimika kulibadili na kujiita Kamikaze, ni msanii
ambaye pengine katika orodha hii anaweza kuwa hafahamiki sana lakini
jamaa anajua kutupia.Staa huyu mavazi yake mara nyingi anakuwa
akipendelea kupiga fulana za kubana na ‘jeans’. Sasa hivi Kamikaze
anayefanya muziki wa Bongo Fleva anakimbiza na Kibao cha Nikikuona.
Izzo Business
Ukimtaja kwa jina la Emmanuel
Simwinga utapata tabu kumtambulisha kwa mashabiki wa Muziki wa Hip Hop
lakini ukimtaja kwa jina lake la kisanaa la Izzo Business utakuwa
umepatia. Jamaa pia hufahamika kama Mr Mbeya City, huyu yupo mstari wa
mbele kulitangaza jina la mkoa huo ambako ndiko alikozaliwa. Mavazi yake
mara nyingi huwa ni suti au ‘jeans’, fulana na sweta jepesi juu yake,
hapo utamtaka.
Jamaa anajitahidi sana kwenye mpangilio wa mavazi, hata kwa wale
ambao hawajafanikiwa kuonana naye ‘live’ basi ukweli wanaupata kupitia
picha za mnato na video za ngoma zake mbalimbali ambazo anaonekana
‘anang’ara’.
Mr Blue
Herry Sameer au Mr Blue kama
anavyofahamika na wengi kupitia kazi yake ya muziki, alianza kuwika
kitambo akiwa bado mdogo baada ya kuachia ngoma yake ya Mr Blue na
kufanikiwa kuwateka watu wengi hasa wanafunzi wa kike.
Jamaa ni mzuri
pia kwenye upangiliaji wake wa mavazi na amekuwa akijitahidi mara kwa
mara kwenda na wakati. Kwa sasa anaishi na mchumba wake anayeitwa Wahida
ambaye amezaa naye mtoto mmoja.
Msanii wa Bongo Fleva aliye juu kwa sasa, Nasib Abdul au Diamond
Platinumz ana jina kubwa sana ndani na nje ya Tanzania kutokana na kazi
zake kukubalika vilivyo lakini pia huwa hakosei kwenye kupangalia mavazi
yake kulingana na sehemu anayokwenda.
Amekuwa na mvuto mkubwa na ni ‘role model’ wa vijana wengi wa sasa
katika uvaaji lakini pia usisahau anajiita Rais wa Wasafi Tanzania,
kweli anafaa hata kungekuwa na cheo zaidi ya rais naamini angefanikiwa
kukamata nafasi hiyo.
Hemed Suleiman ‘PhD’
Ukimtambulisha kama PhD peke
yake kidogo inaweza kuleta ugumu kumfahamu bila kuweka jina Hemed,
ukweli ni kwamba Hemed Suleiman maarufu kama PhD anajua kupiga pamba
hasa katika ‘kumechisha’. Mtazame akiwa amevaa suti iwe nyekundu, bluu
na rangi nyingine mbalimbali, yeye ni mweupe na amekuwa akipendeza
akivaa nguo za aina yoyote.
Huyu ni msanii wa filamu na muziki wa Bongo Fleva ambaye alitokea
kwenye shindano ya Tusker Project Fame. Inadaiwa kuwa katika maisha yake
anapenda sana kula na kwa siku hujitahidi kufukia chakula mara nane na
hadi kufikia saa sita usiku kila siku anakuwa amemaliza kuku wawili na
nusu au watatu.
Gerry wa Rhymes
Jamaa anafahamika zaidi kwa jina
la Gerry wa Rhymes, huyu alianza kufahamika zaidi baada ya kutoa Ngoma
ya I Love You aliyofanya mwaka 2010 tangu hapo akaanza kujikusanyia
mashabiki na sasa yupo juu.Licha ya hivyo, jamaa hayupo nyuma kwenye
suala la kutupia, amekuwa akijitahidi sana kujiweka sawa katika maeneo
hayo na hii imekuwa ikimuongezea sifa popote anapokwenda. Zaidi anapenda
kutupia fulana ya kawaida na jeans wakati mwingine suti mara mojamoja
siyo mbaya kwake.
Bob Junior
Raheem
Nanji maarufu kama Bob Junior anajiita rais wa Masharobaro Tanzania,
yaani wale vijana wote wanaopenda kupendeza huyu ndiyo kiongozi wao mkuu
hiyo ni kwa mujibu wake yeye mwenyewe.Miongoni mwa nguo ambazo pengine
anapenda kuzivaa ni fulana za kubana, jeans na koti lililotengenezwa kwa
kitambaa cha ‘leza’, hapo mtoko wake unakuwa umekamilika.
No comments:
Post a Comment