*Alianza usnichi tangu mwaka
jana lakini safari hii kapiliza
*Hatakiwi kuonekana hata
mtaani kwa Diamond
Mkali
wa wimbo wa Wanjera Omari Nyembo a.k.a Ommy Dimpoz hatakiwi kuonekana kwenye
makazi (state house) ya Mwanamuziki tajiri nchini Nasibu Abdul’, maarufu Diamond
Platinumz kuanzia sasa!
Habari
toka vyanzo vya kuaminika zinasema kuwa urafiki wa Ommy Dimpoz na Diamond
uliingia doa tangu mwaka jana huku chanzo kikielewa kuwa ni tabia ya Ommy
Dimpoz kutaka kuiga kila kitu anachofanya Dimond na wakati mwingine kujifanya yeye ni zaidi ya
mwanamuziki huyo.
Kutokana
na tabia hiyo ndipo Diamond akaanza kumtenga Dimpoz taratibu lakini mambo
yalikuja kuharibika zaidi baada ya Ommy Dimpoz kumtunishia kifua Diamond kwa
kujenga urafiki na ex-girlfriend wake Wema Sepetu huku akiachia picha za
ajabuajabu alizopiga na Wema katika Mitandao ya Kijamii.
“Unajua
Diamond amemsaidia sana Dimpoz kujulikana kimuziki hivyo alipaswa kumheshimu
hata kama kamkosea, sasa Dimpoz baada ya kuona ametoka kimuziki akaanza kutaka
kuishi kama Diamond,wakati mwingine akawa anajifanya yupo juu kuliko Diamond
ndipo Diam0nd akaanza kumtenga taratibu.
“Lakini
badala ya kujirekebisha akaanza kutanua kifua zaidi kwani alipokuja kusikia
Diamond na Wema wameachana na haziivi yeye akajiweka kwa Wema na kuanza
kutengeneza mazingira ya kujionesha kwa
watu kuwa Wema ni demu wake!.
CHANZO: GAZETI LA KIU
No comments:
Post a Comment