Richard Bukos
MAHABA
popote! Licha ya kudaiwa ‘wamemwagana’, wapenzi wawili ambao ni wasanii
ndani ya Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans wameoneshana
mahaba mazito hadharani na kuwaziba midomo waliodhani hawawezi kuwa
pamoja tena.
Ishu hiyo ilinaswa hivi karibuni na ‘kasuku’ wetu maeneo ya Posta
jijini Dar, kulikokuwa na sherehe za utoaji wa tuzo za filamu (TAFA) na
kuwafanya watu wengi kushangaa huku wakionekana kuteta kwa nyakati
tofauti.
“Mmh, hawa wamerudiana kwa mahaba mazito namna hiyo tena? Mbona
tulisikia wameachana sasa naona wamegandana tena,” alisikika msanii
mwingine (jina tunalo).
Hata hivyo, mwandishi wetu alimfuata Ray na kumuuliza kuhusu minong’ono ya wao ‘kutemana’ ambapo alijibu;
“Huyu ndiye mke wangu, hayo mengine achana nayo kabisa.”
No comments:
Post a Comment