Thursday, May 21, 2015

MADAI JINI KABULA AREKODIWA

SHABAAASH! Staa aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’, anadaiwa kurekodiwa mkanda wa ngono na kusambazwa katika mitandao ya kijamii, Amani linakupa stori kamili.
Staa aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’.
Chanzo cha habari hii kimeeleza kwamba, tukio hilo lilitokea hivi karibuni baada ya mtu anayedaiwa kuwa ni mchumba wa staa huyo kumrekodi video hiyo na baadaye walipopishana kauli, akaamua kuisambaza kwa njia ya CD.
“Jana bwana niliona video ya utupu ya Jini Kabula ikiuzwa kitaani kwetu katika CD jambo ambalo ni aibu sana,” alisema mtoa ubuyu wetu, mkazi wa Manzese, jijini Dar.
Amani lilishuhudia baadhi ya picha zinazodaiwa kuwa zilikatwa kutoka katika video hiyo ndipo mwanahabari wetu alipomvutia waya Jini Kabula ili kujua nini kilimsibu hadi akarekodiwa video hiyo.Alisema kwa mazingira ya tukio hilo, anashindwa hata ajibu nini maana haelewi kilichotokea hadi mkanda huo ukasambaa kiasi hicho na kumsababishia matatizo kwa ndugu zake.
“Kiukweli nashindwa hata nikujibu nini maana kama aibu tayari imeshanikuta, hivyo sioni kama naweza kuongea kitu chochote kwa sasa kikanisafisha, kikubwa namwachia Mungu maana sina tena pa kuuficha uso wangu kwa hiki kilichotokea, yaani yamenikuta,” alisema Jini Kabula ambapo alipobanwa zaidi kuhusu aliyemrekodi, alijibu kuwa ni mchezaji wa timu ya Yanga pasipo kumtaja jina.
“Bwana ni mchezaji wa Yanga, alikuwa mtu wangu.”

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...