Wednesday, April 15, 2015

VAI ACHEKELEA KUACHIKA!

MCHEZA filamu anayefanya vizuri nchini, Isabela Francis ‘Vai’ amefunguka na kuchekelea kuachana na mpenzi wake ajulikanaye kwa jina la Boniface Matiku ‘Bonny’, akisema akiwa nyumbani kwa mama yake, ana uhuru wa kuamua chochote, ikiwa ni pamoja na kunywa pombe hata asubuhi.
Mcheza filamu anayefanya vizuri nchini, Isabela Francis ‘Vai’.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko hivi karibuni, Vai alisema zilipendwa wake huyo amekuwa akimuomba msamaha na kudai atamrudishia fedha za televisheni aliyoweka dhamana, lakini hataki kwani nyumbani kwao anaona raha kutokana uhuru alionao.
“Nyumbani ni raha sana, kwani nikitaka kulewa nalewa hata asubuhi, niko huru zaidi ya nilivyokuwa kwa Bonny, hivyo sina mpango wa kurudiana naye kwa sasa japokuwa  ananiomba msamaha sana lakini sitaki, ngoja nipumzike kwanza kwa mama yangu,” alisema Vai.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...