Tuesday, February 24, 2015

LUIS NANI AMWAGA MACHOZI UWANJANI BAADA YA KUFUNGA BAO LA MITA 30..ANGALIA VIDEO

Nani, aliyeinamia chini, akificha uso wenye machozi baada ya kufunga bao kali


Winga wa zamani wa Manchester United, Luis Nani amemwaga machozi uwanjani kwa kuzidiwa na furaha baada ya kufunga bonge la bao, mita 30, wakati timu yake ya Sporting Lisbon ikiichakaza Gil Vicente mabao 2-0 juzi usiku.
Nyota huyo ambaye yupo Lisbon kwa mkopo akitoka Man United, ali-control mpira karibu na eneo la kona kabla ya kuachia fataki kali lililotinga wavuni moja kwa moja. 

Lakini hii si mara ya kwanza kwa mchezaji huyu, na inaonekana ni tabia yake kumwaga chozi, ikikumbukwa aliwahi kumwaga chozi uwanjani  kwenye mchezo baina ya Man United na Livewrpool baada ya Jamie Carragher kumchezea rafu, ilikuwa 2011 na United kulala mabao 3-1 pale Anfield.
Carragher kwa ungwana alimfuata kwenye vyumba vya kubadilishia nguo na kuomba radhi  punde baada ya mchezo kumalizika kabla ya Nani kufunguka kisa cha kulia siku hiyo kwa kusema:
“Nilivyouona mguu wangu kwa mara ya kwanza, nilikuwa msimu wangu ndo basi tena, ndiyo maana nililia sana, siku hiyo.”
Nani kushoto, enzi akiwa Man United akionesha jeraha baada ya kupigwa daruga na Carrager wa Liverpool.

 Angalia video kwa kubofya link hapa chini

http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2964603/Nani-breaks-tears-scoring-Sporting-Lisbon-30-yard-stunner.html#v-4074974010001

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...