Thursday, February 26, 2015

CHID BENZ JELA MIAKA SITA, AKUBALI KULIPA FAINI YA LAKI TISA


Chid Benz (mwenye shati jeupe) baada ya kuachiwa na mahakama.
MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Rashidi Makwilo maarufu kama ‘Chid Benz’, aliyekuwa anatuhumiwa kwa kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin na bangi, leo ameachiliwa huru kwa kulipa faini ya Sh. 900,000.

Katika maelezo ya awali yaliyosomwa na mwendesha mashtaki wa Jamhuri Diana Lukendo, mbele ya Hakimu Warialwande Lema, msanii huyo alimwambia hakimu kuwa mshtakiwa alikamatwa na dawa hizo za kulevya akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, akitaka kusafiri kuelekea mkoani Mbeya.

Hata hivyo mshtakiwa huyo ambaye alikiri kosa mnano tarehe 18 Aprili mwaka huu, leo aliiomba mahakama kumpunguzia adhabu na kwamba asingetumia tena ulevi huo na atawaelimisha vijana wenzake juu ya madhara yake.
…Akiondoka mahakamani.
…Akielekea kwenye gari lililomleta.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...