Bwana
mmoja jijini Mumbai nchini India, amepewa talaka yake, baada ya
kulalamika kuwa hawezi kukata "kiu kubwa" aliyokuwa nayo mke wake ya
kufanya tendo la ndoa.
kwa mujibu wa tovuti ya Metro - Mwanaume huyo akiwa amechoka, alifika
katika mahakama inayoshughulikia masuala ya kifamilia mwezi Januari,
akidai kuwa mke wake amekuwa akimnyanyasa kwa kutaka kufanya tendo la
ndoa, tangu walipofunga ndoa mwaka 2012, na kuwa amekuwa akitumia
'mabavu na udikteta' wakati akitaka jambo lake. Na hakuishia hapo: bwana huyo ameiambia mahakama kuwa mke wake pia alithubutu hata kumpa dawa za kuongeza nguvu, na kutishia 'kutembea' na wanaume wengine kama atashindwa kukata kiu yake kubwa.
Mume huyo akiwa taabani- ambaye amesema amesumbuliwa na maradhi ya kidole tumbo 'appendicitis' kutokana na kutopumzika, alipewa talaka aliyokuwa akidai.
"Kwa kuwa mshtakiwa (mke) hakutokea mahakamani, ushahidi wa mshtaki (mume) haujapingwa. Na hivyo mahakama hii haina budi, ila kukubali ushahidi uliowasilisha" amesema Jaji Laxmi Rao.
No comments:
Post a Comment