Friday, September 12, 2014

Mike Tyson amporomoshea matusi mtangazaji wa kipindi cha TV kilichoruka LIVE

Bingwa wa zamani wa dunia katika mchezo wa masumbwi Mike Tyson alishindwa kuvumilia swali aliloulizwa na mtangazaji wa Canada wa kipindi cha Television kilichokuwa kinaruka Live na kumporomeshea matusi mfululizo.

Mtangazaji huyo, Nathan Downer alikuwa akifanya mahojiano na Mike na alikuwa kwenye kipengele kuhusu mkutano wake na mgombea wa kiti cha Mayor, Rob Ford anaemuunga mkono.

Baada ya maswali mawili matatu, mtangazaji huyo alimuuliza Mike Tyson swali kuhusu sakata lake la kufungwa kwa kosa la ubakaji na hapo ndipo mambo yalipobadilika.

“Baadhi ya wakosoaji wako wanaweza kusema, ‘hizi ni mbio za kuwania kiti cha mayor, tunajua wewe ni mfungwa wa kesi ya ubakaji, hii inaweza kuiumiza kampeni yake (Rob Ford). Utalijibu vipi hilo?” Aliuliza Downer.

Kwanza Tyson alianza kwa kumwambia kuwa hamjui mtu mwingine anaesema hivyo na kwamba amemsikia yeye peke yake akisema hivyo.

“It’s so interesting because you come across as a nice guy but you’re really a piece of shit…“F*ck you.” Alisikika Tyson.

Baada ya sekunde chache aliongeza tena kwa msisitizo hata baada ya kukumbushwa kuwa yuko kwenye kipindi kinachoruka moja kwa moja, “No because you’re a piece a shit, you really are. F*ck you.”
Mtangazaji alijitahidi kuyapotezea yaliyotokea na kuendelea na maswali mengine lakini mambo hayakuwa sawa kabisa.

Baada ya mahojiano hayo, Downer alitweet kuwaomba radhi watazamaji na kwamba kwa upande wake binafsi hana tatizo na alichofanya Tyson.

“No ill will toward Mike Tyson. He lashed out at me and that's okay. Not taking it personally.” Alitweet.

“I'm okay everybody. Unfortuantlely my question hurt Mike Tyson's feelings. That was not my intentions. My apolgies for the language” Inasomeka tweet nyingine ya Downer.

Tyson yuko Canada kwa ajili ya kufanya onesho lake la ‘Mike Tyson: Undisputed Truth’.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...