Saturday, May 17, 2014

MERCY KITUNDU ALIYEACHWA NA MUME MWISLAMU NA KUFIWA NA WANAWE WAWILI SASA MUNGU AMEMPA KIBALI CHA KUZINDUA ALBAMU YAKE YA IMBENI SIFA ZA YESU SIKU YA JUMAPILI 25.05.2014

Mungu aweza kufuta aibu ya mtu na kumuweka wa thamani machoni pa watu. Mercy Charles ni mwaimbaji wa nyimbo za Injili na ni mwalimu wa kufundisha kuimba katika kanisa la K.K.K.T hapa jijini Dar es Salaam. Mwimbaji huyu amepitia mapito makali sana katika maisha yake. Kabla hajaolewa alikuwa Mkristo na alipota mume wa Kislamu aliamua kubali dini yake na kuwa Mwislamu. Katika ndoa yake alibahatika kupata watoto wawili, wa kiume na kike. Mume wake aliamua kuongeza mke wa pili na akamfukuza huyu mke wake wa kwanza ambaye ni Mercy Kitundu. Mbali na kuachwa aliweza kupata pigo lingine na kufiwa na watoto wake wawili.

Mercy Charles Kitundu

Mungu aliweza kumrudisha katika dini yake ya zamani ya KIKRISTO. Akiwa katika dini yake hii aliweza kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji katika kanisa lake, na mpaka sasa anamtumikia Mungu kwa uimbaji.

Siku ya tarehe 25.05.2014 anazindua albamu yake ya IMBENI SIFA ZA YESU pale Mbagala za Zakheem karibu na DAR LIVE ukifika hapoa uliza kanisa la KKKT liko barabarani kabisa lina paa la kijani. Tamasha litaanza saa 7:00 mchana na kuendelea na hakutakuwa na kiingilio chochote.


Katika mahojiano aliyofanya katika ofisi za RUMAFRICA, Mercy Charles Kitundu ameeleza maisha yake kabla na baada ya wokovu, matatizo katika ndoa, waimbaji kutokuwa na mshikamano, watumishi kutokuwa na ushirikiano katika kuujenga mwili wa Kristo, malengo yake katika uimbaji, vikwaza alivyopata katika kuandaa albamu yake, kiasi alichotumia kumaliza albamu yake, maisha yake katika ndoa ya Kiislamu, katoa moni yake na mambo mengi.


Mawasiliano ya Mercy Charle Kitundu ni
+255 756 248 282 au +255 712 502 020
www.mercykitundu.blogspot.com

SASA WAWEZA KUSIKILIZA KILE MERCY KITUNDU ALICHOKIONGEA KATIKA OFISI ZA RUMAFRICA SINZA AFRIKASANA.

WIMBAJI WATAKAO KUWEPO NI KAMA HAWA WAFUATAOKUWEPO KATIKA TAMASHA ZA UZINDUZI WA ALBAMU YAKE NI KAMA WAFUATAO.

Kutakuwa na waimbaji wengi sana kama BAHATI BUKUKU, MADAM RUTI, ENOCK (ZUNGUKA ZUNGUKA), JULIETH DOUGRAS, SARAH MVUNGI, MAGRETH SEMBUCHE, MC JERRY, MERCY JACOB CHENGULA, FURAHA ISAYA, TUMAINI NJOLE, LEA AMOSI na wengine wengi.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...