Sunday, April 20, 2014

BATULI: NILIFURAHI KUKUTA MAGAZETI YA PENDWA BUNGENI




Mwanadada mrembo kutoka Bongo Movies, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ pozini.

MWANADADA mrembo kutoka Bongo Movies, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ amefunguka kuwa alifurahi kukuta magazeti Pendwa ya Global Publishers ndani ya mjengo wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Akipinga stori na paparazi wetu, Batuli alisema aliyaona magazeti hayo hivi karibuni alipokuwa amekwenda mjengoni humo kuwawakilisha wasanii katika Bunge la Katiba akiwa ameambatana na Rais wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), Saimon Mwakifwamba na mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’.

’’Magazeti yote ya siku utayapata palepale ila nilifurahi zaidi kuona magazeti Pendwa ndiyo yamepewa kipaumbele zaidi, wauzaji huyaweka mbele kuonyesha vichwa vya habari na ndiyo maana waheshimiwa wanajua sana stori za wasanii,” alisema Batuli.

Magazeti Pendwa yanayochapishwa na Kampuni ya Global Publishers Ltd ni Ijumaa Wikienda linalotoka kila Jumatatu, Uwazi (Jumanne), Risasi Mchanganyiko (Jumatano), Amani (Alhamisi) Ijumaa (Ijumaa) na Risasi Jumamosi (Jumamosi).

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...