Monday, February 10, 2014

RAY, CHUCHU HANS PENZI LAO HALINA KIFICHO TENA



Ray na Chuchu wakijiachia.

MAMBO hadharani! Penzi ‘hoti’ la mastaa mahiri wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa sasa limekuwa kama la njiwa kwani mara nyingi kila sehemu wapo pamoja na hakuna kificho tena.

Chanzo chetu makini kilieleza kuwa mastaa hao wamekuwa wakionekana pamoja mara nyingi na hivi sasa inadaiwa kuwa wanaishi pamoja huku wakiwa na mtoto wa Chuchu aitwaye Danzel.
Mpashaji wetu huyo alizidi kudai kuwa kutokana na mapenzi hayo kukolea siku hadi siku, juzikati baadhi ya ndugu wa mastaa hao walianza vikao vya chini kwa chini ili kuhakikisha mwaka huu wasanii hao wanafunga ndoa lakini haijajulikana kama watafungia kanisani au msikitini kwa kuwa wana dini tofauti.
“Yaani sasa hivi hakuna siri hata chembe, ni fulu kujiachia. Mara nyingi wapo pamoja kila sehemu yaani kama njiwa,” kilisema chanzo chetu.


Chanzo hicho kilizidi kudai kwamba mara nyingi Ray na Chuchu wanapenda kwenda kuogelea na kujiachia kama mke na mume kwenye hoteli moja maarufu (jina linahifadhiwa) iliyoko maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar huku wakijifotoa picha za kumbukumbu.

Baada ya kujazwa ‘info’ hizo na kumwagiwa picha za mastaa hao, gazeti hili lilimtafuta Chuchu kisha kumuuliza kuhusiana na penzi lake na Ray kuwa ‘shatashata’ ambapo alifunguka kuwa kama kuna mtu anawaona wakiwa pamoja ni kwa sababu hivi sasa eti wanaandaa ‘sinema’ yao wawili.
Alipotafutwa Ray ili kuulizwa kuhusiana na ishu hiyo, simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa kwa muda wa nusu saa.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...