Sunday, August 18, 2013

UZINDUZI WA SERENGETI FIESTA 2013 KIGOMA USIPIMEEE...




Msanii wa muziki wa kizazi kipya Cassim Mganga akiimba jukwaani mbele ya maelfu ya wakazi wa Kigoma ndani ya uwanja wa Lake Tanganyika.

Sehemu ya umati wa watu waliofurika ndani ya uwanja wa Lake Tanganyika usiku wa kuamkia leo.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Neylee akiimba kwa hisia kwenye jukwaa la tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Sehemu ya umati wa watu waliofurika kwenye uwanja wa Lake Tanganyika usiku wa kuamkia leo wakiburudika na wasanii wa Serengeti Fiesta 2013.

Palikuwa hapatoshi ndani ya uwanja wa Lake Tanganyika.

Mwanamuziki mahiri wa muziki wa Dansi, Christian Bella akikamua jukwaani.

Ni shangwe tu ndani ya uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

Yaani hapatoshi kabisa, wakazi wa Kigoma wamecharuka na burudani murua kabisa ya tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Rachael kutoka THT, akionesha umahiri wake wa kutumbuiza jukwaani.

Washabiki wa tamasha la Fiesta wakifuatilia kwa makini burudani hizo.

Peter Msechu na madansa wake wakikamua vilivyo katika tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Shilole Mohamed na madansa wake wakiwachengua vilivyo wakazi wa Kigoma, waliojitokeza kwa wingiusiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta ndani ya uwanja wa Lake Tanganyika.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...