Friday, August 2, 2013

KUMBE BARNABA ALIMTEMA SHILOLE BAADA YA KUMTWISHA ZIGO ZA KUMLELEA WATOTO WAKE, ...!



Baada ya siku nyingi kupita tangu Shilole na Barnaba watemane,imebainika kuwepo kwa siri kubwa zilisababisha wawili hao watemane ....

Chanzo cha karibu na Barnaba kimedai kuwa sababu zilizosababisha wawili hao kutemana ni pale shilole alipodanganya umri wake na kumwachia Barnaba jukumu la kumlelea watoto wake...

"Suala la kulea watoto wasio wa kwake lilikuwa ni gumu sana kwa Barnaba kwani wakati huo ndo kwanza alikuwa anaanza maisha na hakuwa na uwezo wa kumhudumia mtu na wanae"..Kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kiliendelea kufunguka kuwa Shilole ndiye aliye mtongoza Barnaba kwa staili ya kumdanganya umri huku akimweleza kuwa swala la watoto wake lilikuwa linasimamiwa na baba yao.

Habari zinadai kwamba, baada ya Barnaba kuingizwa mkenge, penzi lao lilikuwa kwa kasi sana huku Shilole akijitahidi kuuficha ukweli kwa muda mrefu.

"Cha ajabu ni kwamba, kadri siku zilivyozidi kusonga mbele, Shilole alijisahau na kuanza kumwachia mzigo wa kuilea familia yote..

"Aidha, Shilole aliusahau uongo wake na akajichanganya kutoa historia ya maisha yake katika gazeti moja la udaku ambako alitaja umri wake halisi huku akisimulia jinsi alivyobakwa hadi kupata mimba .Jambo hilo lilimstua sana Barnaba"..Kilisema chanzo hicho na kuongeza:

"Kipengele cha kubakwa kilimchanganya sana Barnaba akawa anajiuliza, kama alibakwa na kupata mtoto,matunzo ya mtoto anayapataje kwa mtu aliyembaka

"Tukio hilo lilo lilimfanya Barnaba apoteze imani na ndipo alipoanza alipoanza kutafuta visa vya kumtema Shilole"

Shilole alipotafutwa kuzungumzia suala hilo hakuweza kutoa ushirikiano wa kutosha.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...