Wednesday, July 31, 2013

ROSE NDAUKA ANASWA AKIPAPASWA NDANI YA GARI KABLA YA KUPELEKWA HOTELINI



Rose Ndauka au Aisha anaweza kuwa ameitia najisi funga yake baada ya kunaswa akiingia hotel moja iliyoko kinondoni jijini Dar kwa kile kilichoelezwa ni kwenda kuivunja amri ya sita na mwanamziki wa bongo fleva Nassoro Ayoub "Nasry" au Tajiri Boy

Rose ambaye alisilimu mwaka jana na kupewa jina la Aisha baada ya kuchumbiwa na mwanamziki mwasisi wa kundi wa TNG Squad, Malik Bandawe, alifumwa na kamera za wakazi wa jirani na hoteli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita.....

Shuhuda wa tukio hilo amedai kwamba majira ya mchana kweupe gari aina ya Toyota Mark X lenye rangi nyeusi liliwasili kwenye viunga vya hoteli hiyo na kusimama kwa takribani dakika 10 kisha likaondoka na kwenda kupaki sehemu nyingine ambapo ni umbali mfupi toka hotelini hapo...

Kitendo hicho kiliibua mashaka miongoni mwa watu hasa kutokana na vioo vya gari hilo kuwa tinted hivyo kutowaonesha waliokuwemo ndani...

"Walipoondoka na kupaki palipojificha tuliamua kuwasogelea ili tujue ni akina nani

"Baada ya muda, kioo cha dereva kilishushwa kidogo, tukamuona dogo anayefanana na Diamond akiwa anampapasa demu aliyekuwa pembeni yake...

"Tulipoona hivyo, tulidhana mnyamwezi ameamua kumaliza mambo yake ndani ya gari, hivyo tukaziweka simu zetu standby kwa ajili ya kushuhudia" alisema shuhuda huyo

Baada ya muda, mlango wa kulia ulifunguliwa kisha wakamuona dogo aliyetambuliwa kwa jina la Nasry

"Kumbe hakuwa Diamond,alikuwa ni dogo Nasry.Tulipotupa jicho ndani, tulihamaki kumuona Rose Ndauka akibadili nguo na kujitanda baibui.

"Nadhani alifanya hivyo ili watu wasimjue pindi atakaposhuka kwenye gari maana aliposhuka tu, waliongozana na dogo Nasry kwa mwendo wa kasi hadi ndani...


"Toka walipoingia ndani hadi walipotoka iliwachukua kama masaa matatu hivi.Wakati wa kutoka, Nasry alilifuata gari hadi mlangoni na kisha Rose akaingia na kutokomea"...Kilimalizia kusimulia chanzo hicho

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...