Thursday, July 18, 2013

"NIPO TAYARI KUPIGANA NA JACK WOLPER ENDAPO ATAENDELEA KULITUMIA JINA LANGU KUJIPATIA UMAARUFU"...BABY MADAHA



Staa wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph ‘Baby Madaha’ ameomba pambano la ngumi dhidi ya Jacqueline Wolper ili waweze kumaliza ubishi wa bifu lao.


Akipiongea na mwandishi wetu, Baby alisema amechoshwa kusikia tambo za mpinzani wake huyo hivyo kama kweli ni mwanamke, wakutane kwa ngumi ili amuoneshe cha mtema kuni.


“Asiniambie mimi natafuta kiki, mimi ni msomi kuliko yeye, arudi shule au akauze vipodozi. Najua kuimba, kuigiza na ni msomi yeye anaweza hayo?

"Kimsingi naomba pambano nimtoe manundu.Nipo tayari kupigana naye ili nimshikishe adabu,” alisema Baby Madaha.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...