Tuesday, July 9, 2013

NANDO NA FEZA KESSY WAENDELEA KUPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA NDANI YA BIG BROTHER......HAKUNA ALIYEINGIA KIKAANGONI


Wiki hii Watanzania na mashabiki wa shindano la Big Brother Africa hawana haja ya kuwa wasiwasi ya kuwaokoa washiriki wao kwakuwa Nando na Feza Kessy wako safe.
Kilichobaki ni kuvuta tu viti virefu na kuendelea na bata huku tukiwaangalia wengine wakihaha kuokoa washiriki wao.

Hata hivyo Evictions ya wiki hii inatarajiwa kuwa ya aina yake tangu show ianze hasa kwakuwa waliotajwa kuondoka ni washiriki ngangari.

Ni nani kati ya Cleo, Natasha, Pokello, Selly, Melvin na Annabel anayeweza kubwaga manyanga kwenye mchezo huo wa ‘kufukuzana’? Afrika itaamua.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...