Wednesday, February 6, 2013

MZEE MAJUTO AMHOFIA JOTI



Mzee Majuto

Nguli wa Filamu za kuchekesha nchini mzee Majuto a.k.a King Majuto alifunguka kwamba baada ya Swahiba wake kipendi marehemu Sharo Milionea kufariki, anamkubali sana msanii Joti. Mzee Majuto alisema hayo wakati akijibu swali aliloulizwa na Mtangazaji wa Kipindi cha Mikasi kinachorushwa kupitia EATV SALAMA JABIR, akijibu swali hilo Mzee majuto alisema "Baada ya kifo cha Sharo Milionea ambae nilikuwa namtumia kama Meneja wangu na pia kufanya nae matangazo mbalimbali, msanii ninayemkubali ni JOTI ambaye kwa sasa yuko nyuma yangu na pengine huko baadae anaweza kuwa juu yangu kisanii.'

Pamoja na kujibu maswali yake kwa ufasaha mkubwa bila kusahau kuweka ucheshi wa kuchekesha ambapo kila aliyetizama kipindi hicho hakusita kicheka, Mzee Majuto alitoa ombi wa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mh.Jakaya Mrisho Kikwete aweze kumpa msaada wa trecta ya kulimia mabapo alisema anatamani sana kuwa mkulima kwani mashamba tayari anayo ila anahitaji msaada wa trecta ili aweze kulima kilimo cha kisasa kwa sababu kwa umri wake hawezi kutumia jembe la mkono.

Baada ya kauli ya Mzee Majuto kwa Joti hii ndio kauli ya Joti aliyoitoa katika ukurasa wake wa facebook:  
NAHESHIMU SANA KAZI ZA WASANII WENZANGU.. PIA. NILIJISIKIA FARAJA KWA MTU KAMA KING MAJUTO KUITAMBUA SANAA YANGU.. HESHIMA KWA KING MAJUTO NA KWA WASANII NA. MASHABIKI ZANGU WOTE WANAONIELEWA NACHOKIFANYA.. One lav

Joti

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...