Tuesday, February 5, 2013

MHESHIMIWA SUGU AMSHUKIA ROMA KWA KUMTAJA KWENYE 2030:

Sugu
Mwana muziki ambaye kwa sasa ni Mheshimiwa kwa tiketi ya ubunge alioupata Mbeya  Joseph Mbilinyi alimaarufu kama Mr 11 au Sugu ameonyesha wazi kukerwa na msanii mwenzie Roma kwa kile alichodai Roma ana kurupuka na hajui anachokifanya.

Akizungumza nda ya EATV Katika kipindi cha friday Night Live Sugu amesema kuwa msanii huyo anapaswa kuijua misingi ya hip hop na pia Sugu amemuonya na kumtaka roma awe muangalifu na anachokiandika na kukitowa kwa jamii na sio kukurupuka kama mtu aliyestuliwa toka usingizini.

Sugu amesema yeye ni mfuasi wa hip hop hivyo ukitaka kuwa mwana hip hop lazima uzame ndani sana ili ukiandika kitu uwe na uhakika nacho na si kufanya kama Roma anavyofanya.Namtahadharisha bwana mdogo awe muangalifu na anachokiandika na si kukurupuka hip hop ina misingi yake na ni lazima uzame ndani sana maana hip hop ni maisha na ukweli mtupu, pia aelewe hip hop ni sauti ya kumkombowa mnyonge sasa unapoimba mambo ambayo huna uhakika nayo haipendezi maana utakuwa hujaisaidia jamii husika alisema sugu.

Roma
Katika wimbo  huo wa 2030 kuna kipande kina sema pesa ndio imemaliza vita yaRuge na Sugu kitu ambacho kimeonyesha kumkera Sugu na kusema kuwaRoma anakurupuka na kuandika asichokijua maana kwa mstari huo tu umefanya niaamini kila achoandika hana anachokijua maana mstari huu unanihusu na hakuna ukweli juu ya alichokiimba.

Sugu amemtaka Roma kusikiliza nyimbo walizoimba kaka zake ili zimuongoze katika sanaa yake amesema asikize nyimbo kama za profesa jay,afande sele,solo thang atagunduwa kuwa zilikuwa ni harakati za uhakika mfano mdogo amesema asikilize miss Tanzania ya Solo Thang atajua anachomaanisha.

  Roma alipotafutwa kujua amejisikiaje baada ya mheshimiwa kuchukizwa na wimbo wake Roma alisema Sugu ni kaka yake na anaamini kama kuna baya atamuita na atamrekebisha alipoulizwa  kama alikuwa na uhakika kuwa vita ya Sugu na Ruge imemalizwa na pesaR

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...