Friday, February 22, 2013

DOTNATA NDANI YA ULIMWENGU WA WAFU.



Dotnata mtayarishaji wa filamu ya Ulimwengu wa Wafu.
 
MWIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood Husna Poshi ‘Dotnata’ amesema kuwa amerudi rasmi katika tasnia ya filamu baada ya kuwa nje ya Tanzania, Dotnata alikuwa safarini Naijeria katika shughuli zake za kila siku pia
msanii huyo amesema kuwa hivi sasa kuna filamu yake kali na ya kusisimua ya Ulimwengu wa Wafu.

“Najaribu kufanya utafiti kuhusu soko la filamu zetu, ikiwa pamoja na kuwatumia wasanii kutoka sehemu mbalimbali, kwa mfano katika filamu yangu ya Ulimwengu wa Wafu nimeweza kuwashirikisha wasanii kutoka Kongo, Burundi na Tanzania, filamu zijazo niwashirikisha wasanii waliofanikiwa sana kutoka Naijeria na kwingineko,”anasema Dotnata.

Filamu ya Ulimwengu wa Wafu ni filamu iliyorekodiwa Tanzania na Burundi ikiwashirikisha wasanii kama Patcho Mwamba, Hisany Muya ‘Tino’, Dotnata, Lumole Matovolwa ‘Bigg’ filamu hiyo imeongozwa na Moses Mwanyilu ‘Uncle Mo’ na kuandaliwa na Tanganyika Entertainment, filamu hiyo inasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.

Biggie Mwigizaji wa filamu Swahiliwood, pia ameshiriki katika filamu ya Ulimwengu wa Wafu,

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...