Thursday, December 27, 2012

MSHINDI WA UNIQUE MODELKUIBUKA LEO


Ile siku iliyosubiriwa na watanzania wengi kutaka kujua nani ataibuka mshindi wa shindano la kumsaka mwanamitindo wa mwaka mwenye sifa za pekee nchini Tanzania imewadia
Homa ya shindano imezidi kupanda ikiwa usiku wa leo atajulikana nani atavishwa taji la unique model of the year 2012 taji lenye heshima katika tasnia ya mitindo nchini Tanzania.
Jumla ya washiriki kumi na mbili wanapanda kujwaani kuwania taji hilo ikiwa fainali zake zitafanyika katika ukumbi wa maraha New Maisha club uliopo Oysterbay jijini Dar.
Wanaowania taji hilo ni Vestina Jax,Judith sangu,Amina Ayoub,Catherine Masumbigana,Elizabeth Pertty,Elizabeth Boniface,Vivian Gilbert ,Darline Mmari , Zeenath Habibb,Sandra Suleiman,Cecilia Emmanuel,Magreth Msafiri.
Mratibu wa shindano hili Bwana Methusela Magese amewaomba watanzania wajitokeze kwa wingi siku  wa leo kwani kuna mambo mazuri ya kufurahisha ikiwemo burudani ya muziki wa bendi toka kwa mashujaa,ngoma za asili na bongo flava kwa kiingilio cha Tshs 15,000/= tu.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...