Saturday, November 24, 2012

IRENE UWOYA, FLORA MVUNGI.....BIFU UPYA!!!!!!!!!!!!



MSANII wa bongo movie na mziki Flora Mvungi ameibuka na kudai kuwa ana majina 10 ya wabunge ambao tayari wameshatembea na Irene Uwoya na anaweza kumuanika wakati wowote atakapojisikia.

Wasanii hawa waliwahi kuwa katika bifu zito, lakini sasa linaonekana kuchukua sura mpya, ambapo inadaiwa kuwa Mvungi tayari ameshapanga kuyatoa majina hayo na anasubiri wakati muafaka ili aweze kuanika ishu hiyo.

Mvungi ambaye ni mchumba wa msanii wa muziki wa kizazi kipya H-Baba, amedai kuwa anajua mengi kuhusu Uwoya ambayo jamii haijapata nafasi ya kuyajua.

Msanii huyo akiongea na mwandishi wetu amesema kuwa kwenye list hiyo wapo wabunge wengine ambao wanaweza kuwa ni umri wa baba yake lakini kutokana na tabia zake za hajali. Aliongeza kuwa kuna kipindi wakati alipokuwa hana ujauzito alikuwa akipanga safari za kwenda Dodoma mara kwa mara pamoja na Uganda huko alikuwa akienda kwa ajili ya vigogo hao.

“Naweka wazi kwani hana shukrani na nipo katika mchakato wa kuanika picha zake zote alizopiga na wabunge hao alipokuwa akila bata,” alidai.

Baada ya hiyo pia aliizungumzia safari ya Uwoya ya Uingereza kuwa alichukuliwa na bwana wa kizungu, ingawa hapa nchini alitoa habari za uongo kuwa anaenda kwa ajili ya kutafuta soko la filamu.

Mwandishi wetu alimtafuta Uwoya ili ajibu ishu hiyo, lakini hakuweza kuzungumza kwa undani na kudai kuwa anajua ni kwa nini Mvungi ametoa kauli hizo chafu, zenye lengo la kumfanya ili aonekana mbaya, na kuongeza kuwa hajawahi kutembea na mbunge yoyote wa Tanzania hii.

Pia alikana kuwa hakuchukuliwa na mzungu na kupelekwa nje kwani alienda kwa ishu zake za kikazi, lakini kama Mvungi anataka kuanzisha bifu yuko tayari kulipokea ka kudai Mvungi ni mtoto mdogo ambaye hajui analolizungumza.

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...