Tuesday, November 27, 2012

HIVI NDIVYO ALIVYOTUTOKA SHARO MILLIONEA .



Marehemu Sharomilionea enzi za uhai wake

Taarifa kuhusu kifo cha Msanii wa maigizo na Mziki wa Bongo fleva kufariki zimasamba nchi nzima masaa machache yaliopita.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari ni kwamba amepata uthibitisho kutoka kwa diwani Makame Seif ambaye ni rafiki yake wa karibu sana wa Marehemu Hussen Ramadhani Mkiete maarufu kama Sharo Millionea amepata ajali mida ya saa mbili eneo la maguzoni Tanga na amefariki dunia papo hapo.

Polisi walitambua ni Sharo Millionea kwa vitambulisho vyake na picha moja ya passport aliokuwa nayo mfukoni ambavyo kwa sasa viko na polisi.
Diwani huyu alimfahamisha mwandishi kuwa Sharo Millionea aliumia vibaya sana kichwani, kifuani na kwenye mikono.
Pia Mjomba wa marehemu amethibitisha kuwa Sharo Millionea atazikwa Tanga na asubuhi ya leo ratiba ya msiba ingetolewa.
Ndugu na marafiki wa Sharo wameanza kwenda hospitalini baada tu ya taarifa hizi kuwafikia. Familia ya Sharo iliwasiliHospitali ya Teule ya Tanga mara baada ya kupata taarifa hizo.

 
Hii ndiyo gari aina Toyota Harrier yenye namba T278 BVR iliyopinduka na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha msanii Sharo milionea jana usiku mishale ya saa mbili.











No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...